Katika kuadhimisha Wiki ya Utumishi wa Umma mwaka 2025, Chuo Kikuu Mzumbe Ndaki ya Dar es Salaam kimeendesha mafunzo mahsusi kwa watumishi wake kuhusu uwekezaji na usawa wa kijinsia, yakiwa na lengo la kuboresha ufanisi kazini na maandalizi ya maisha baada ya kustaafu. Akifungua rasmi maadhimisho hayo Juni 17, 2025, …
Read More
Chuo Kikuu Mzumbe kinashiriki katika mashindano ya kimataifa ya mdahalo yajulikanayo kama Social Justice Debate Arusha ambayo yanalenga kujadili masuala ya haki ya kijamii katika muktadha wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Mashindano hayo yameanza tarehe 14 Juni 2025 na yanatarajiwa kufikia tamati tarehe 15 Juni 2025, yakifanyika jijini Arusha, Tanzania …
Read More
Wanataaluma wa Kitivo cha Sayansi za Jamii katika Chuo Kikuu Mzumbe wamepatiwa mafunzo ya siku moja kuhusu uandishi wa mapendekezo yanayoweza kushinda ufadhili wa miradi ya utafiti pamoja na ufadhili wa kutekeleza miradi isiyo ya kuutafiti. Vilevile, wanataaluma hao walipata kuelezwa umuhimu wa afya na ujumuishaji wa anuai za kijamii …
Read More
Ndaki ya Mbeya ilipata heshima kubwa ya kupokea ujumbe maalumu kutoka Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), tarehe 13 Juni 2025. Ziara hiyo ililenga kuimarisha ushirikiano kati ya chuo na UNDP katika nyanja za maendeleo endelevu, ubunifu, na kuwajengea uwezo watumishi pamoja na wanafunzi. Ujumbe huo uliongozwa na …
Read More
Chuo Kikuu Mzumbe kimeanza mchakato wa kuanzisha Stashahada ya Umahiri ya Ubunifu wa Kijamii na Ujasiriamali kupitia Mradi wa ADVANCE (Advancing Social Innovation and Entrepreneurship through Postgraduate Education in East Africa). Warsha ya wadau wa mradi huo imefanyika leo tarehe 12 Juni 2025 katika Kampasi Kuu ya Chuo Kikuu Mzumbe, …
Read More
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe, Prof. William Mwegoha, amefanya ziara ya kikazi Ndaki ya Dar es Salaam tarehe 9 Juni 2025 na kuzungumza na wanafunzi katika kikao kilicholenga kukagua maendeleo yao, kusikiliza changamoto, maoni, pamoja na kutoa dira ya uongozi wa chuo kuhusu masuala mbalimbali yanayogusa ustawi wa elimu …
Read More
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe, Prof. William Mwegoha, amekutana na Watumishi wa Ndaki ya Dar es Salaam tarehe 9 Juni 2025 katika kikao maalumu kilicholenga kujadili masuala mbalimbali ya maendeleo ya chuo na ustawi wa watumishi. Akizungumza katika kikao hicho, Prof. Mwegoha aligusia masuala yanayohusu hali ya watumishi na …
Read More
Kupitia Makubaliano ya Ushirikiano kati ya Chuo Kikuu Mzumbe na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), Ndaki ya Mbeya imezindua rasmi Klabu ya Miliki Bunifu tarehe 6 Juni 2025. Klabu hiyo ni ya kwanza ya aina yake kuzinduliwa nchini Tanzania. Uzinduzi huo ulihudhuriwa na wanafunzi, wahadhiri pamoja na …
Read More
Chuo Kikuu Mzumbe, Ndaki ya Dar es Salaam, kimeandaa Mhadhara wa Umma uliohusu Simulizi kwa ajili ya Kubadili Maisha katika Jamii "Story Telling for Social Change". Mhadhara huo ulilenga kuwasaidia kuwa wabunifu, kuanzisha taasisi, pamoja na kuwa na mawazo mbadala ya kusaidia jamii kukabiliana na changamoto mbalimbali. Akizungumza Juni 6, …
Read More
Chuo Kikuu Mzumbe kimeadhimisha Siku ya Mazingira Duniani, Juni 5, 2025 kwa njia ya kipekee kwa kutoa elimu ya udhibiti wa taka za plastiki kupitia shughuli mbalimbali za kimazingira zilizofanyika katika Kampasi Kuu ya Chuo hicho, Morogoro. Maadhimisho hayo yaliyoandaliwa na Klabu ya Wanafunzi ya Kutunza Mazingira ya Chuo Kikuu …
Read More
Chuo Kikuu Mzumbe Ndaki yake ya Dar es Salaam, tarehe 3 Juni, 2025 kimeendesha mafunzo kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari Kijitonyama Sayansi iliyopo Kata ya Kijitonyama, Wilaya ya Kinondoni kuhusu matumizi sahihi ya maktaba na maktaba mtandao ikiwa ni sehemu ya jitihada za taasisi hiyo kushiriki katika utoaji wa …
Read More
Chuo Kikuu Mzumbe Ndaki ya Mbeya, kwa kushirikiana na Vodacom Tanzania, kimeendesha Mhadhara kwa Umma tarehe 31 Mei, 2025 uliojikita katika kujadili masuala ya uwekezaji kidigitali na elimu ya fedha kwa maendeleo ya wanafunzi wa vyuo vikuu. Mada kuu ya mhadhara huo ilikuwa “Ufunguaji wa Fursa kwa Vijana (Wanafunzi wa …
Read More
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe, Profesa William Mwegoha, amekutana na wanafunzi wa Kampasi Kuu ya Morogoro tarehe 2 Mei 2025 kwa lengo la kuwasikiliza, kupokea maoni na kuwapa mrejesho kuhusu masuala ya kitaaluma, kijamii na kiutawala. Mkutano huu ni sehemu ya juhudi za uongozi wa Chuo kuimarisha mawasiliano na …
Read More
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe Profesa William Mwegoha amekutana na kuzungumza na wafanyakazi wote wa Kampasi Kuu Morogoro ambapo alielezea mafanikio mbalimbali yaliyopatikana chuoni hapo ikiwemo ongezeko la wafanyakazi, marekebisho ya miundombinu mbalimbali ya Chuo ikiwemo uboreshaji nyumba za wafanyakazi, barabara za ndani na uwekaji wa taa za barabarani. …
Read More
Chuo Kikuu Mzumbe kupitia Skuli ya Biashara (SoB), chini ya Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET), kimeendesha Mhadhara wa Umma tarehe 30 Mei, 2025 Kampasi Kuu Morogoro. Mhadhara huo uliwalenga wafanyakazi na wanafunzi, hususan wa fani ya Ununuzi na Ugavi, kwa lengo la kuwaelimisha kuhusu namna …
Read More
Tarehe 28 Mei, 2025, Rasi wa Ndaki ya Mbeya, Prof. Henry Mollel alizindua Mfululizo wa Semina za Uwasilishaji wa tafiti. Tukio hili kubwa linalenga kujenga jukwaa muhimu la kuwasilisha mapendekezo ya tafiti, kukuza utamaduni wa kutoa tafiti na machapisho bora miongoni mwa wanafunzi wa Ndaki ya Mbeya na Chuo Kikuu …
Read More
Chuo Kikuu Mzumbe kimepokea ugeni kutoka Ubalozi wa India nchini Tanzania tarehe 26 Mei 2025, katika ziara iliyoongozwa na Mkuu wa Utawala, Katibu wa pili anayeshughulikia ITEC, Elimu na Afya kutoka Ubalozi wa India, Bw. Rajnish Kumar akiambatana na Msaidizi wa Usalama kutoka Ubalozi wa India, Bw. Godse Nanaso. Ugeni …
Read More
Chuo Kikuu Mzumbe kimeandaa mafunzo ya uthibiti ubora kwa wakuu wa idara za taaluma, waratibu wa uthibiti ubora na waratibu wa programu za kitaaluma, yaliyofanyika Kampasi Kuu, mkoani Morogoro na kujumuisha wawakilishi kutoka Kampasi za Mbeya na Dar es Salaam. Mafunzo hayo yaliyofunguliwa rasmi tarehe 26 Mei 2025 na Kaimu …
Read More
Chuo Kikuu Mzumbe kupitia Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET), chini ya Kitengo cha Ubunifu, Ujasiriamali na Mahusiano ya Kitasnia, kimeandaa warsha ya siku tano kwa ajili ya kuimarisha uwezo wa ubunifu kwa wanafunzi wa Chuo Kikuu Mzumbe – Kampasi Kuu. Warsha hiyo ilianza rasmi tarehe …
Read More
Chuo Kikuu Mzumbe kupitia Mradi wa Elimu ya Juu na Mageuzi ya Kiuchumi (HEET), kimeendesha warsha maalum ya siku mbili kuanzia tarehe 27 hadi 28 Mei 2025, Hoteli ya Morena yenye lengo la kuwawezesha watafiti na wahadhiri wake kuandika mapendekezo ya miradi ya utafiti yenye uwezo wa kupata ufadhili mkubwa …
Read More
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe Prof. William Mwegoha amefanya ziara ya kikazi Ndaki ya Mbeya na kuzungumza na wanafunzi tarehe 26 Mei 2025. Lengo likiwa ni kukagua maendeleo ya wanafunzi, kusikiliza maoni na changamoto kutoka kwa wanafunzi pamoja na kutoa dira na mwelekeo wa Chuo kuhusu masuala muhimu yanayohusu …
Read More
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe, Prof. William Mwegoha amekutana na kufanya mazungumzo na watumishi wa Chuo hicho Ndaki ya Mbeya ikiwa ni sehemu ya utaratibu wa kutembea ndaki za Chuo kujadili mambo ya kimkakati na maendeleo ya chuo. Prof. Mwegoha akiambatana na sehemu ya Menejimenti ya Chuo hicho kutoka …
Read More
Chuo Kikuu Mzumbe kwa kushirikiana na Mradi wa Elimu ya Juu na Mageuzi ya Kiuchumi (HEET) kimeendesha Warsha ya kuwasilisha matokeo ya utafiti kwa wadau mbalimbali ambao wana mnasaba na tafiti zilizofanywa. Warsha hiyo inalenga kuwasilisha na kujadili matokeo ya tafiti mbalimbali zilizofanywa na watafiti kutoka Chuo hicho, pamoja na …
Read More
Mashindano ya Vitivo ya mwaka 2025 Chuo Kikuu Mzumbe yamefunguliwa rasmi Mei 24, 2025 katika viwanja vya michezo vya chuo, yakihusisha michezo mbalimbali kwa lengo la kukuza vipaji, mshikamano na afya miongoni mwa wanafunzi. Mashindano haya yanayojumuisha vitivo na skuli mbalimbali yanachochea ushirikiano, ari ya ushindani na burudani. Katika ufunguzi …
Read More
Chuo Kikuu Mzumbe kimeingia katika ushirikiano rasmi na Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) kwa kusaini hati ya makubaliano tarehe 23 Mei 2025, inayolenga kuimarisha maeneo ya tafiti, mafunzo kwa vitendo, na ubadilishanaji wa uzoefu kati ya pande hizo mbili. Makubaliano hayo yalisainiwa rasmi na Makamu Mkuu wa Chuo …
Read More
Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) imeendesha mhadhara wa umma mnamo tarehe 23 Mei, 2025 katika Kampasi Kuu ya Chuo Kikuu Mzumbe, ukilenga kuelimisha jamii ya wanachuo kuhusu nafasi ya ALAT katika kuimarisha utawala bora na ufanisi wa serikali za mitaa nchini. Mhadhara huo, ulioratibiwa na Idara ya Menejimenti …
Read More
Chuo Kikuu Mzumbe kimezindua rasmi Kituo cha Ubora kwa Ufundishaji na Ujifunzaji wa Kibunifu (Centre of Excellence in Innovative Teaching and Learning - COEITL), katika hafla iliyofanyika Mei 20, 2025, Kampasi Kuu ya Chuo mkoani Morogoro. Uzinduzi huo umeongozwa na Makamu Mkuu wa Chuo, Prof. William A. Mwegoha, ambapo amepongeza …
Read More
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe Prof. William Mwegoha, ametembelea na kukagua miradi ya maendeleo na uboreshaji wa miundombinu katika Kampasi Kuu ya Chuo Kikuu Mzumbe, Morogoro. Ziara hiyo ilifanyika tarehe 20 Mei 2025, ambapo aliambatana na viongozi mbalimbali wa Menejimenti ya Chuo. Katika ziara hiyo, Prof. Mwegoha alitembelea miradi …
Read More
Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe ambaye pia ni Naibu Makamu Mkuu wa Chuo anayeshughulikia Taaluma,Tafiti na ushauri Prof. Hawa Tundui amesema Chuo Kikuu Mzumbe kinaandaa mwongozo wa matumizi ya akili mnemba (Artificial Inteligence) kwa kuwa matumizi ya teknolojia hiyo hayakwepeki katika dunia ya sasa na kwamba yana umuhimu …
Read More
Katika kuhakikisha kuwa wanafunzi wa Chuo Kikuu Mzumbe wanahitimu elimu ya juu wakiwa na uwezo wa kujiajiri, kuanzisha biashara endelevu ili kuchangia kikamilifu maendeleo ya uchumi wa taifa, Chuo Kikuu mzumbe kupitia mradi wa HEET kimeandaa warsha maalum ya kuamsha na Kulinda bunifu na Ujuzi wa Biashara kwa wanafunzi wa …
Read More
Mafunzo kuhusu fursa mbalimbali za kijasiriamali yametolewa mwishoni mwa wiki na wadau mbalimbali wa ujasiriamali katika muendelezo wa kusherehekea siku ya Chuo kikuu Mzumbe na kambi ya ujasiriamali. Mkurugenzi wa TAOTIC bw Kiko Kiwanga akielezea kazi mbalimbali zinazofanywa na taasisi yake kama njia ya kumsaidia kijana mjasiriamali, alisema; wao wamejikita …
Read More
Chuo Kikuu Mzumbe kupitia Kitengo cha Ubunifu, Ujasiriamali na Uhusiano wa Kitasnia, kimeadhimisha Siku ya Mzumbe na Kambi ya Ujasiriamali katika Kampasi Kuu ya Morogoro, tarehe 7 Mei 2025 na kuhudhuriwa na washiriki kutoka sekta mbalimbali za elimu, biashara, uwekezaji na taasisi za serikali. Akizungumza wakati wa tukio hilo, Kaimu …
Read More
Wanafunzi na wahitimu wa vyuo mbalimbali walikusanyika tarehe 11 Mei 2025, Chuo Kikuu Mzumbe Kampasi Kuu Morogoro kwenye tukio la Majadiliano Kuhusu Fursa na Mbinu za Ajira (Career Fair), lililofanyika kwa ushirikiano kati ya Niajiri Platform na Association Internationale des Étudiants en Sciences Économiques et Commerciales (AIESEC). Tukio hili lililenga …
Read More
Katika kusherehekea siku ya Chuo Kikuu Mzumbe na Kambi ya wajasiriamali ya chuo hicho iliyopamwa na mambo mbalimbali ikiwemo hafla ya chakula jioni iliyojumuisha wafanyakazi, wadau mbalimbali wa chuo hicho wakiwemo wajasiriamali waliosoma na wanaosoma chuoni hapa imefanyika tarehe 7 Mei 2025 Kampasi Kuu Morogoro. Akifungua hafla hiyo Kaimu Makamu …
Read More
Chuo Kikuu Mzumbe kimeanza rasmi Kambi ya Ujasiriamali kwa shamrashamra za bonanza la michezo lililofanyika tarehe 7 Mei 2025, likihusisha michezo ya aina mbalimbali ambayo ilileta burudani na mshikamano miongoni mwa wanafunzi na watumishi wa chuo. Bonanza hilo lilifunguliwa rasmi na Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Prof. Hawa Tundui, ambaye …
Read More
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Exaud Kigahe (Mb.), amekipongeza Chuo Kikuu Mzumbe kwa kuwatengenezea mazingira wanafunzi wa chuo hicho yanayohamasisha ubunifu, kujifunza mbinu za Ujasiriamali, uwekezaji na Biashara wakati wakiendelea na masomo yao chuoni hapo na hivyo kuwaandaa vyema kujiajiri na kutatua changamoto ya ajira na kuwawezesha kuchangia …
Read More
Mzumbe University has actively participated in the launch of Tanzania Internationalisation Strategies for Higher Education (TANZIE) project, held at the University of Alicante, Spain, and the University of Saarland, Germany. The TANZIE project aims to enhance the global engagement of Tanzania’s Higher Education Institutions (HEIs) by strengthening institutional capacity for …
Read More
Chuo Kikuu Mzumbe kimefanya Mkutano wa Kwanza wa Baraza la Tano la Wafanyakazi uliolenga kuimarisha mazingira bora ya kazi na ustawi wa watumishi wa chuo hicho. Mkutano huo umefanyika leo Tarehe 29 Aprili 2025 katika Ukumbi wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) na kuongozwa na Makamu Mkuu wa …
Read More
Mratibu wa Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET) wa Chuo Kikuu Mzumbe, Prof. Eliza Mwakasangula, akiambatana na waratibu wengine wa mradi, amefanya ziara ya ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa Kampasi mpya ya Chuo Kikuu Mzumbe katika eneo la Kata ya Gombero, Wilaya ya Mkinga, Mkoa …
Read More
Warsha maalumu ya watoa huduma (wadau) wa Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET) imefanyika Kampasi Kuu, Chuo Kikuu Mzumbe, tarehe 21 Machi 2025, ikiwakutanisha waratibu wa mradi wa HEET Chuo Kikuu Mzumbe na watoa huduma mbalimbali kwa lengo la kuwaelimisha katika maeneo ya Miundombinu, Mazingira, Jinsia, …
Read More
Katika hatua muhimu ya safari yake ya kitaaluma, Bw. Mwandu Jiyenze, mwanafunzi wa Shahada ya Uzamivu (PhD) kutoka Kitivo cha Sayansi za Jamii, Chuo Kikuu Mzumbe, amefanikiwa kutetea tasnifu yake kwa mafanikio makubwa. Utetezi huo umefanyika leo, 17 Machi 2025, katika Kampasi Kuu ya Chuo Kikuu Mzumbe, Morogoro, mbele ya …
Read More
Chuo Kikuu Mzumbe kupitia kurugenzi yake ya afya kimezindua huduma ya kipimo cha ‘Ultra Sound’ ambayo imeanza kutolewa katika kituo cha afya cha chuo hicho kinachohudumia Wanafunzi, wafanyakazi na Wananchi wa kata ya Mzumbe na maeneo Jirani. Akizindua huduma hiyo Machi 19,2025 Kaimu Makamu Mkuu wa chuo kikuu Mzumbe ambaye …
Read More
Wafanyakazi wa Chuo Kikuu Mzumbe, Ndaki ya Dar es Salaam wameshiriki bonanza maalum la michezo lililofanyika katika Fukwe za Empire, Bagamoyo, Mkoani Pwani, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha mshikamano, afya na mahusiano bora kazini kwa ajili ya kuongeza tija katika utendaji wa majukumu yao ya kila siku. Bonanza …
Read More
Chuo Kikuu Mzumbe kimeratibu na kuwakutanisha Wadau katika warsha ya kujadili matokeo ya utafiti wa miradi ya maendeleo vijijini na mabadiliko ya kiikolojia ‘Collaborative Researches Centers – CRC for Future Rural Afrika’ unaofadhiliwa na Baraza la utafiti la Ujerumani na kutekelezwa kwa pamoja kati ya vyuo vikuu vya Born na …
Read More
Katika kusimamia misingi ya utoaji wa elimu bora, wanataaluma kutoka Idara ya Sayansi za Jamii na Insia ya Ndaki ya Mbeya wameanda na kuendesha semina ya siku moja kwa wanafunzi wa Shahada ya Awali ya Rasilimali Watu(BHRM). Semina hiyo ilifanyika Tarehe 24 April, 2025 katika ukumbi wa Nkurumah Ndaki ya …
Read More
Chuo Kikuu Mzumbe Ndaki ya Dar es Salaam kwa kushirikiana na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), kimeendesha semina maalumu kwa wanafunzi wake, hususan wa Shahada ya Kwanza, iliyolenga kujenga uelewa kuhusu masuala ya rushwa, viashiria vyake, athari na mbinu za kuikabiliana. Akifungua semina hiyo katika kituo cha …
Read More
Chuo Kikuu Mzumbe kinaendelea na maandalizi ya Siku ya Mzumbe na Kambi ya Ujasiriamali itakayofanyika kuanzia tarehe 07 hadi 09 Mei 2025, Kampasi Kuu Morogoro. Akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano uliofanyika tarehe 25 Aprili 2025 – katika Ukumbi wa Multimedia wa Kituo cha Ubora katika Ufundishaji na Ujifunzaji …
Read More
Chuo Kikuu Mzumbe Ndaki ya Dar es Salaam kimeendesha mafunzo maalum kwa wanafunzi wake kwa lengo la kuwaongezea ujuzi katika maeneo muhimu ikiwemo ujasiriamali wa kisasa, matumizi ya teknolojia mpya, na mbinu za kuwavutia waajiri wa ndani na nje ya nchi. Akizungumza wakati wa mafunzo hayo yaliyofanyika katika Kituo cha …
Read More
Chuo Kikuu Mzumbe kimeweka historia kwa kushiriki na kung’ara katika mashindano mashuhuri zaidi duniani ya usuluhishi wa migogoro ya kibiashara – "The 32nd Willem C. Vis International Commercial Arbitration Moot" yanayofanyika jijini Vienna, Austria, barani Ulaya. Mashindano hayo yanahusisha vyuo zaidi ya 400 kutoka kote duniani, yamewakutanisha wanafunzi wa sheria …
Read More
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe Prof. William Mwegoha ameongoza ujumbe wa Chuo ukijumuisha Naibu Makamu Mkuu wa Chuo – Taaluma, Utafiti na Ushauri, Prof. Hawa Tundui, Mtiva wa Kitivo Cha Sheria, Dkt. Sarafina Bakta, Mkuu wa Kitengo cha Uthibiti Ubora, Dkt. Lawrencia D. Mushi na Mkurugenzi wa Shahada za …
Read More
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe Prof. William Mwegoha ameungana na wananchi wa Wilaya ya Mvomero katika mapokezi ya Mbio za Mwenge wa Uhuru yaliyofanyika mwishoni mwa wiki katika kijiji cha Sangasanga, Kata ya Mzumbe. Tukio hilo muhimu limefanyika katika eneo la ofisi ya Mtendaji wa Kijiji cha Sangasanga na …
Read More
Bi. Alphonsina Ambrosi, Mhadhiri Msaidizi katika Idara ya Lugha na Stadi za Mawasiliano, Kitivo cha Sayansi za Jamii amekuwa mmoja wa washiriki wa Kongamano la Lugha za Kiafrika huko Marekani katika Chuo Kikuu cha Pittsburgh kuanzia tarehe 10-12 Aprili 2025. Katika Kongamano hilo, Bi. Alphonsina amewasilisha makala yake ya kitaaluma …
Read More
Wafanyabiashara wadogo wanaofanya biashara zao ndani ya Chuo Kikuu Mzumbe wamenufaika na mafunzo ya muda mfupi yaliyoandaliwa na Idara ya Uhasibu na Fedha kwa lengo la kuwaongezea uelewa juu ya masuala ya kodi, tozo pamoja na misingi ya uhasibu na fedha. Mafunzo hayo yamefanyika tarehe 11 Aprili 2025 na kufunguliwa …
Read More
Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe – Taaluma, Utafiti na Ushauri Prof. Hawa Tundui, amefungua rasmi warsha ya Uwasilishaji wa Tafiti na Udhamini wa Masomo ya Shahada ya Uzamivu (PhD unaofadhiliwa na Mradi wa SAfA. Akizungumza wakati wa ufunguzi wa warsha hiyo iliyofanyika chuoni Mzumbe, Prof. Tundui alieleza kuwa …
Read More
Chuo Kikuu Mzumbe kupitia Kitivo cha Sayansi na Teknolojia, Idara ya Masomo ya Kompyuta, kimeendesha Mhadhara wa Umma uliojikita katika mada ya "Kushamiri kwa Teknolojia ya Akili Unde na Namna Inavyoathiri Maisha ya Kila Siku". Mhadhara huo umefanyika tarehe 09 Aprili 2025, chini ya uratibu wa Mradi wa AI4STEM (AI-Driven …
Read More
Bw. Wilfred Kavishe, mwanafunzi wa Shahada ya Uzamivu (PhD) kutoka Skuli ya Biashara ya Chuo Kikuu Mzumbe, ameandika historia kwa kutetea kwa mafanikio tasnifu yake ya utafiti leo tarehe 9 Aprili 2025, Kampasi Kuu, Morogoro. Utetezi huo ulifanyika mbele ya jopo la watahini lililoongizwa na Prof. Hawa Tundui. Mada ya …
Read More
Chuo Kikuu Mzumbe kimezindua rasmi mradi wa AI4STEM, ambao unaolenga kuboresha elimu ya Sayansi, Teknolojia, Uhandisi na Hisabati (STEM) kupitia matumizi ya Teknolojia ya Akili Unde (AI). Uzinduzi huu umefanyika tarehe 08 Machi 2025 katika Kampasi Kuu, Morogoro. AI4STEM — kifupi cha AI-Driven Inclusive STEM Learning in Tanzania — ni …
Read More
Chuo Kikuu Mzumbe Ndaki ya Dar es Salaam kwa kushirikiana na Ubalozi wa Norway nchini Tanzania wametoa semina ya usawa kijinsia katika masuala ya uongozi na biashara kwa wanafunzi wa Chuo hicho ikiwa ni sehemu ya mpango mkakati wa Chuo wa kuwajengea uwezo wanafunzi ili waweze kuwa wabobezi katika nyanja …
Read More
Chuo Kikuu Mzumbe kimeshiriki kikamilifu katika Kikao Kazi cha Utekelezaji wa Mradi wa HEET (Higher Education for Economic Transformation), kinachoratibiwa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia (MoEST) kwa kushirikiana na Benki ya Dunia. Kikao hiki kinalenga kutathmini maendeleo ya utekelezaji wa miradi inayotekelezwa kupitia HEET katika taasisi mbalimbali za …
Read More
Chuo Kikuu Mzumbe ni Taasisi ya umma ambayo ilianzishwa kwa mujibu wa Sheria ya Chuo Kikuu Mzumbe Na. 21 ya mwaka 2001. Sheria hiyo ilifutwa na Sheria ya Vyuo Vikuu Na. 7 ya mwaka 2005 ambayo inasimamia masuala yote yanayohusu Elimu ya vyuo Kikuu nchini Tanzania. Kwa sasa, Chuo kinatekeleza …
Read More
Chuo Kikuu Mzumbe kupitia Kitengo cha Udahili pamoja na Kitengo cha Mawasiliano na Masoko kimetembelea Shule ya Sekondari Bwawani iliyopo Wilaya ya Chalinze, Mkoa wa Pwani, na Shule ya Sekondari Sokoine Memorial iliyopo Wilaya ya Mvomero, Mkoa wa Morogoro. Ziara hii imelenga kuwaelimisha wanafunzi kuhusu fursa mbalimbali za elimu zinazopatikana …
Read More
Katika jitihada za kutafuta suluhisho bunifu kwa changamoto za tabianchi, wadau wa mazingira, wajasiriamali na wataalamu wa sekta mbalimbali wamekutana katika Jukwaa la Ubunifu wa suluhisho endelevu kwa changamoto za Tabianchi (CLIMATHON) ambalo linawezesha vijana kubuni na kuendeleza mawazo kwa maendeleo endelevu. Tukio hilo limekuwa fursa kwa wabunifu chipukizi kubuni …
Read More
Chuo Kikuu Mzumbe, kupitia Skuli ya Biashara, kimeandaa mafunzo maalumu kuhusu Huduma kwa Wateja na Usimamizi wa Utoaji wa Huduma Bora, yaliyofanyika tarehe 26 Machi 2025 Kampasi Kuu Morogoro. Mafunzo haya yamewaleta pamoja washiriki kutoka sekta mbalimbali kwa lengo la kuboresha ufanisi wa utoaji wa huduma kwa wateja na kujenga …
Read More
Ikiwa ni katika utekelezaji wa jukumu mojawapo la wanataaluma wa Chuo Kikuu Mzumbe ambalo ni Kutoa Ushauri Kitaaluma, Kurugenzi ya Huduma za Jamii imeandaa na kuendesha warsha ya siku mbili ya ujuzi katika utoaji ushauri upande wa wanataaluma. Warsha hii ya siku mbili imeanza kutolewa kwa wanataaluma wa Ndaki ya …
Read More
Wafanyakazi wa Chuo Kikuu Mzumbe, Ndaki ya Dar es Salaam, wamesisitiza dhamira yao ya kusaidia jamii kwa kutoa shauri za kitaaluma zinazolenga kuboresha maendeleo ya jamii na sekta mbalimbali. Haya yalibainika katika mafunzo ya uandishi wa ushauri za kitaaluma yaliyofanyika 21 Machi 2025, katika Ndaki hiyo jijini Dar es Salaam. …
Read More
Chuo Kikuu Mzumbe chenye Mkataba wa Makubaliano na Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) wa kutoa mafunzo ya mifumo tumizi ya TEHAMA nchini kwa Taasisi za Umma, kimeendesha mafunzo kwa vitendo ya mfumo wa Ofisi Mtandao na Mfumo wa Barua pepe za Serikali kwa watumishi wa Umma kwa kada za Afisa …
Read More
Chuo Kikuu Mzumbe kupitia Skuli ya Biashara kimeendesha mafunzo maalum ya uwezeshaji wa kifedha kwa mafundi wa fani mbalimbali katika Kata ya Mzumbe. Mafunzo haya ni sehemu ya juhudi za chuo kurudisha kwa jamii (Corporate social responsibility)kwa kuhakikisha wananchi wananufaika moja kwa moja na maarifa yanayotolewa chuoni hapo. Akifungua mafunzo …
Read More
Haya yalisemwa tarehe 18 machi kwenye warsha iliyoandaliwa na Chuo Kikuu Mzumbe, Kampasi Kuu Morogoro, ambapo wanawake kutoka sekta mbalimbali walikusanyika kwa lengo moja: kuvishinda vikwazo vinavyowazuia kufanikiwa katika masuala ya uongozi na utafiti. Warsha yenye kaulimbiu “Kuvunja Vikwazo: Kuchochea Hatua kwa Wanawake katika Masuala ya Uongozi na Utafiti” iliwaleta …
Read More
Katika kuendeleza dhima ya kuimarisha Ushirikiano na Mahusiano ya Kitasnia, Chuo Kikuu Mzumbe kimesaini Hati ya Makubaliano ya Ushirikiano na Chama cha Wafugaji Tanzania. Hafla ya utiaji saini imefanyika tarehe 18 Machi 2025, Kampasi Kuu Morogoro ikijumuisha viongozi wa Chuo Kikuu Mzumbe na viongozi wa Chama cha Wafugaji Tanzania. Akizungumza …
Read More
Mwanafunzi wa Shahada ya Uzamivu, Bw. Juma Zuberi Homera, ameandika historia muhimu katika safari yake ya kitaaluma baada ya kutetea kwa mafanikio tasnifu yake ya Uzamivu (PhD), Utetezi wa tasnifu hiyo umefanyika leo tarehe 17 Machi 2025, Kampasi Kuu ya Chuo Kikuu Mzumbe, Morogoro. Bw. Homera amefanya utetezi tasnia yake …
Read More
Chuo Kikuu Mzumbe kimeshiriki katika kikao cha tathmini ya Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET) kati ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na Waratibu wa Mradi wa HEET kutoka Taasisi 22 za Elimu ya Juu nchini Tanzania. Kikao hiki kinalenga kupokea na kujadili maendeleo ya …
Read More
Wahadhiri kutoka Skuli ya Biashara ya Chuo Kikuu Mzumbe wamefanya ziara maalumu katika Shule za Sekondari Morogoro na Kola Hill kwa lengo la kuwaelimisha wanafunzi kuhusu fursa za masomo zinazotolewa chuoni hapo, hususan katika kozi za Ujasiriamali na Masoko. Wahadhiri hao walitoa elimu kuhusu umuhimu wa elimu ya biashara katika …
Read More
Chuo Kikuu Mzumbe kimetoa mafunzo elekezi kwa watumishi wake wapya, wakiwemo wale waliopata ajira mpya na waliokaribishwa kupitia uhamisho kutoka taasisi nyingine, ili kuwajengea uelewa kuhusu taratibu za utumishi wa umma na matumizi sahihi ya mifumo ya TEHAMA inayotumika Serikalini. Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, Mkurugenzi wa Kitengo …
Read More
Miaka 25 ijayo itafafanuliwa na Dira ya Maendeleo ya Tanzania (TDV) – 2050. TDV 2050 haitabadilisha tu sera za kitaifa, bali pia itatoa mwongozo wa utekelezaji wa mipango ya taasisi, sekta mbalimbali, mikakati na miradi ya maendeleo. Haya yamesemwa tarehe 26 Februari 2025 na Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya …
Read More
Chuo Kikuu Mzumbe kimeshiriki katika uandaaji wa Semina ya Kuendeleza Uwezo wa Tathmini Tanzania 2025: Mustakabali wa Tathmini, semina hii imefanyika katika Chuo Kikuu cha Ardhi Dar es Salaam, Tanzania kuanzia tarehe 25 hadi 27 Februari 2025. Tukio muhimu limewaleta pamoja watunga sera, watafiti, wasomi na wataalamu wa maendeleo kujadili …
Read More
Wajumbe wa Menejimenti ya Chuo Kikuu Mzumbe wameanza rasmi mafunzo maalumu ya siku tatu yanayohusu Usimamizi wa Sheria ya Ununuzi wa Umma (PPA), Matumizi ya Mfumo wa NeST (National e-Procurement System) na Usimamizi wa Mikataba. Akifungua mafunzo hayo Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo, Prof. Allen Mushi amewataka washiriki kuzingatia mafunzo …
Read More
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe Prof. William Mwegoha amesema ameridhishwa na kasi ya ujenzi wa Kampasi mpya ya Chuo hicho katika Wilaya ya Mkinga Mkoa wa Tanga. Prof. William Mwegoha ameyasema hayo leo Februari 26, 2025 mara baada ya kufanya ziara ya kikazi ya kukagua maendeleo na hatua za …
Read More
Mwanafunzi wa masomo ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) kutoka Chuo Kikuu Mzumbe Bi. Prisila Emmanuel Kessy ameibuka mshindi na kutwaa tuzo mbili za ubunifu kwenye masuala ya TEHAMA zilizoandaliwa na Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kupitia Tume ya TEHAMA. Katika hafla ya ugawaji wa tuzo hizo …
Read More
Chuo Kikuu Mzumbe kupitia Taasisi ya Taaluma za Maendeleo (IDS) chini ya Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET), kimeandaa warsha kuhusu mabadiliko ya tabianchi. Warsha hii imefanyika Kampasi Kuu, Morogoro, tarehe 12 Februari 2025, kwa ajili ya kuongeza uelewa wa jamii kuhusu athari za mabadiliko ya …
Read More
Chuo Kikuu Mzumbe kupitia Mradi wa Kuimarisha utoaji wa Huduma za Msaada wa Kisheria kupitia Maudhui mafupi ya KITEHAMA hii leo umekabidhi vifaa vyenye thamani ya takriban Milioni Thelathini kwa taasisi ya Legal Vision Organisation (LEVO) ya Lushoto - Tanga) na Morogoro Paralegal Centre (MPLC -Morogoro) katika hafla iliyofanyika Wilaya …
Read More
Chuo Kikuu Mzumbe mshindi wa pili, tuzo za walipa kodi bora kwa mwaka 2023/2024 divisheni ya walipa kodi wakubwa. Tuzo hizo zimetolewa na Mamlaka ya Mapato Tanzania jana 08/02/2025 katika Hotel ya Morena - Morogoro. Tuzo hiyo imepokelewa na Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Prof. Allen Mushi.
Read More
Chuo Kikuu Mzumbe kupitia Idara ya Usimamizi wa Mifumo ya Afya iliyopo chini ya Skuli ya Utawala wa Umma na Menejimenti kimeandaa kongamano la mwisho wa muhula (End-of-Semester Student Forum) kwa ajili ya wanafunzi wa idara hiyo. Kongamano hilo lililenga kuwaunganisha wanafunzi na kuwaelimisha kuhusu masuala mbalimbali ya kitaaluma na …
Read More
Chuo Kikuu Mzumbe kupitia Kitivo cha Sayansi za Jamii kimewezesha wanafunzi wa mwaka wa pili wa Shahada ya Sayansi ya Uchumi (Bachelor of Science in Economics) kushiriki katika ziara ya mafunzo katika Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA). Ziara hiyo ilihusisha wanafunzi kutoka katika programu tatu za shahada ambazo …
Read More
Kamati ya Uendeshaji wa Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET) Chuo Kikuu Mzumbe imefanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa ndaki mpya ya Tanga. Ziara hiyo iliongozwa na Naibu Mratibu wa Mradi wa HEET Chuo Kikuu Mzumbe, Prof. Hawa Tundui, ambaye alisema kuwa kamati imefanya …
Read More
Chuo Kikuu Mzumbe kupitia Skuli ya Biashara, (SoB) kimewezesha wanafunzi wa mwaka wa pili wa Shahada ya Kwanza ya Ununuzi na Mnyororo wa Usambazaji kufanya ziara ya mafunzo katika Kiwanda cha Sukari Mkulazi Holding Company, kilichopo Mbigiri, Wilaya ya Kilosa, mkoani Morogoro. Ziara hiyo, iliyofanyika tarehe 30 Januari 2025, chini …
Read More
Chuo Kikuu Mzumbe kimeungana na Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Morogoro katika Maadhimisho ya Wiki ya Sheria 2025 kwa kushiriki kikamilifu kutoa elimu na ushauri kwa wananchi katika masuala mbalimbali ya kisheria. Uzinduzi wa maadhimisho haya umefanyika tarehe 25 Januari 2025 kwa matembezi ya aina yake yaliyoanzia Kituo Jumuishi …
Read More
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe Prof. William Mwegoha amesema Mzumbe iko mbioni kuanzisha Kampasi mpya Mkoani Mwanza. Prof. Mwegoha ameyasema hayo tarehe 13 Januari 2025 mara baada ya kukutana na kufanya mazungumzo na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda. Amesema Chuo kimepata ekari 221 katika Wilaya ya …
Read More
Chuo Kikuu Mzumbe kwa kushirikiana na UDOM, SUA, UDSM na MUHAS kimeandaa Kongamano la Tatu la Kitaifa la Taaluma za Maendeleo ili kujadili mwelekeo wa maendeleo ya kijamii yaliyopita, ya sasa na yajayo, ili kukidhi mahitaji ya dunia inayokabiliwa na changamoto za teknolojia na mabadiliko ya tabianchi. Akifungua rasmi kongamano …
Read More
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametunukiwa Shahada ya Udaktari wa Heshima katika Uongozi ya Chuo Kikuu Mzumbe ambapo katika hotuba yake amesema kuwa kiongozi ni mtumishi anayeendeleza ya jana, anayebuni, kuibua na kutekeleza ya leo na akaacha ya kuendelezwa kwa ajili ya kesho. …
Read More
Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe na Rais Mstaafu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein amepokea taarifa ya maendeleo ya Chuo iliyowasilishwa na Makamu Mkuu wa Chuo, Prof. William Mwegoha leo tarehe 06 Novemba, 2024 Zanzibar. Katika kuwasilisha taarifa hiyo …
Read More
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda akutana na Mwenyekiti wa Baraza na Menejimenti ya Chuo Kikuu Mzumbe. Kikao hiki kimefanyika tarehe 01 Novemba 2024, Mkoani Dodoma.
Read More
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais - Muungano na Mazingira Mhe. Khamis Hamza Khamis ameitaka jamii kuwa mstari wa mbele katika kutoa elimu ya kutunza na kuhifadhi mazingira ili kuwa na kizazi chenye uelewa na kuthamini mazingira hususan uchumi wa bluu. Ameyasema hayo leo tarehe 22/10/2024 wakati wa ufunguzi …
Read More
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe Prof. William Mwegoha tayari amejiandikisha kupiga kura katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024. Kaulimbiu ya Uchaguzi huo ni "Serikali za Mitaa, Sauti ya Wananchi, Jitokeze kushiriki Uchaguzi"
Read More
On September 25, 2024, the United Nations Development Programme (UNDP) Resident Representative, Mr. Shigeki Komatsubara, made a significant visit to Mzumbe University (MU) Main Campus, signaling a growing partnership between the university and UNDP aiming at advancing professional competencies and nurturing talents to youth in Tanzania who can manipulate the …
Read More
Chuo Kikuu Mzumbe kimeendelea kung'ara kwenye jukwaa la kimataifa baada ya kutwaa tuzo mbili za maandiko bora katika Kongamano la 6 la Kimataifa la Utekelezaji na Mnyororo wa Ugavi kwa Afrika (ACOSCM) lililofanyika Bishkek, Kyrgyzstan. Kongamano hilo liliandaliwa na Shirika la Kuehne Foundation na liliwaleta pamoja wataalamu wa ugavi kutoka …
Read More
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe Prof. William Mwegoha amesema Mzumbe iko tayari kushirikiana na wadau wengine wa ndani na nje ya nchi katika kubadilishana uzoefu katika maeneo ya taaluma na tafiti. Prof. Mwegoha amesema hayo leo Agosti 14, 2024 wakati wa hafla ya kusaini hati ya makubaliano kati ya …
Read More
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe, Prof. William Mwegoha ameelezea Mchango wa Sekta ya Elimu ya juu katika kuimarisha sekta ya Kilimo katika maendekeo endelevu. Prof. Mwegoha amefafanua hayo leo katika mahojiano ya moja kwa moja kupitia EFM na TVE Tanzania kupitia kipindi cha Joto la Asubuhi leo tarehe 08 …
Read More
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan,ameahidi kuendelea kuunga mkono jitihada zinazofanywa na Menejimenti ya Chuo Kikuu Mzumbe katika kukiendeleza chuo hicho kwa kutumia fedha za makusanyo ya ndani kuanzisha miradi ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa majengo mapya na upanuzi wa kampasi zake ili …
Read More
Mkuu wa Wilaya ya Tanga Mheshimiwa James Kaji amewaalika wakazi wa Mkoa wa Tanga kutembelea banda la Chuo Kikuu Mzumbe katika maadhimisho ya Wiki ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu yanayoendelea kwenye Viwanja vya Shule ya Popatlal Jijini Tanga ili kupata uelewa wa kozi na huduma nyinginezo zinazotolewa na Chuo hicho …
Read More
Mzumbe University invites applications from qualified Tanzanians and non-Tanzanians for admission into various Certificate and Diploma programmes offered by the University for the 2024/2025 academic year. The university offers eight (8) Certificate Programmes and seven (7) Diploma Programmes. Three (3) of the seven (7) Diploma Programmes are offered at the …
Read More
The Directorate of Research, Publications and Postgraduate Studies (DRPS), Mzumbe University invites applications for admission to the postgraduate programmes (Masters and Doctoral degree Programmes) for the 2024/2025 academic year from qualified candidates. NB: THE APPLICATION WINDOW FOR MASTER’S DEGREE PROGRAMMES WILL OPEN ON 22ND APRIL, 2024 AND THE DEADLINE FOR …
Read More